vendredi 22 juillet 2011

20 % mara ya kwanza Burundi kwa ajili ya uzinduzi wa albam ya "Sugu Jay"

Baada ya wasani kadhaa kufika apa Burundi na kufanya vizuri kupitiya ma show, msani 20 % ukipenda umuite "sura mpya miguu ya zamani" atafika kwa mara ya kwanza apa Burundi. Msanii huo najulikana sana apa burundi kupitiya nyimbo zake kadha kama "money", "mama neema", "ya nini malumbano" na zingine, na kupitiya piya filamu yake " Furaha gani" ambayo imekubalika sana apa Burundi. Msanii huyo atakuwa apa Burundi siku ya Idil Fitri, ku uzinduzi wa albam ya msani "Sugu Jay" ikibeba jina la "First love" ambao hadi sasa tayari ilisha record nyimbo kadhaa kama " Karo", "First love", " Prity girl", " Prouder", nyimbo hizo zinafanya vizuri kupitiya uwanja huu wa muziki wa Burundi. Siku hiyo tena, msani huyo "Sugu Jay" akiwa piya ni mcheza filamu, akiongoza kundi la "Buja art" atazinduwa filamu yao ya pili ikijulikana kama " Kisa demu".

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire